GAZA CITY, Gaza
MAPIGANO yameanza upya katika eneo la Gaza baada ya kutulia kwa wiki moja.
Wapalestina 10 wameuawa hadi sasa wakiwemo mtoto na mke wa Kamanda wa jeshi la Hamas, Mohammed Deif.

Kuanza upya mapigano hayo kumevuruga mazungumzo ya amani yaliyokuwa yakiendelea nchini Misri ambapo Israel imetangaza kuwaondoa wajumbe wake wote waliokuwa wakishiriki.
Hamas imewarudisha wanajeshi wake 2,000 walioruhusiwa kurudi nyumbani baada ya kukubaliana kusimamishwa kwa mapigano hayo wiki iliyopita.
Hadi sasa karibu Wapalestina 2,000 wameuawa tangu kuanza kwa mashambulizi hayo Julai 8, mwaka huu wakati Israel ikipoteza watu 63.
No comments:
Post a Comment